Wednesday 7 February 2018

ALIYEMUAPISHA ODINGA YAMKUTA MAZITO

Miguna na Odinga.
MWANASHERIA maarufu wa nchini Kenya Miguna Miguna aliyemuapisha Raila Odinga, amefukuzwa nchini Kenya (deported) na kupelekwa Canada, chini ya uangalizi wa serikali.

Taarifa kutoka Kenya ambazo zimethibitishwa na mwanasheria wake zinasma kwamba Miguna aliondolewa nchini kwa ndege ya KLM iliyoondoka na Nairobi, saa 4 usiku.
Tukio hilo limetoka muda mfupi baada ya mahakama ya juu ya nchini humo kuamrisha kufutwa kwa kesi zake zote alizofunguliwa, baada ya waendesha mashtaka na pplisi kushindwa kufika mahakamani, na kumpeleka Miguna.
Odinga akiapa.
Kitendo cha Miguna kuwa deported kimelalamikiwa na baadhi ya wanaharakati, wakisema hawamtendei haki, kwani mwanasheria huyo ni raia wa Kenya na mzaliwa wa Kenya.
Ifahamike kwamba Miguna ana uraia wa nchi mbili ikiwemo Canada na Kenya, uraia alioupata wakati akisoma na kufanya kazi kule kama mwanasheria.

Miguna alikamatwa na Polisi Ijumaa ya wiki iliyopita kwa kosa la kumuapisha Raila Odinga kitendo ambacho ni kinyume na sheria, lakini aliachiwa kwa dhamana na kukamatwa tena kabla hajatoka.
Share:

RIHANNA ATIKISA SENEGAL


Msanii maarufu duniani wa muziki wa Pop Robyn Rihanna Fenty maarufu kama Rihanna, amewasili nchini Senegal licha ya watu wa dini nchini humo kupinga ujio wake, wakimtuhumu kuwa ni mwanachama wa Iluminati (Freemason).

Akiwa nchini Senegal sambamba na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, Rihanna ameshiriki kwenye kongamano kubwa la kuchangia kuinua sekta ya elimu nchini humo, na kusema kwamba hawataacha kufanya hivyo mpaka pale watakapohakikisha kila mtoto anakwenda shule na kupata elimu bora.

“Haya ni mapambano ambayo hatutaacha kwamwe kupambana mpaka pale kila mtoto wa kiume na mtoto wa kike ana uwezo wa kupata elimu”, alisikika Rihanna akisema hivyo.

Kwa upande wa Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, amesema suala la kuchangia elimu sio la kujiamualia, ni suala nyeti na la loazima.

Kwenye mkutano huo uliofanyika Dakar nchini Senegal, Rihanna sambamba na Rais Emmanuel Macron wa Ufarsansa, waliwataka viongozi wa dunia na mashirika makubwa wanyotoa misaada kuongeza juhudi za kuinua elimu kwa nchi zinazoendelea barani Afrika.
Share:

Friday 12 January 2018

MANENO YA MPOKI BAADA YA KUONA STUDIO ZA WCB

Mchekeshaji wa kundi la original comedy Mpoki ameamua kufanya utani kuhusiana na headquaters mpya za WCB baada ya kufanya vice versa na kile alichokipost Diamond Platnumz kwa kuonesha nyumba ya udongo katika page yake ya instagram na kusema ni studio za wachafu wakati Diamond alisema ni studio za wasafi.
Mpoki aliandika caption inayosema “tutaonana, hii ndio headquarters ya wachafu fm na tv kama kawa tukutane sehemu ya kuosha magari tutaonana hivi karibuni”
Share:

UVCCM: INAWEZEKANA TUSIFANYE KAMPENI 2020

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Taifa, Kheri James amesema kuwa CCM haina sababu ya kufanya kampeni katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 badala yake kuna kila sababu ya kupita bila kupingwa kutokana na uimara wa CCM na serikali yake.
 Kheri ameyasema hayo wakati akizungumza na timu mbalimbali za kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani wa Kata ya Kimandolu mkoani Arusha kutoka jumuiya za CCM.
 Kheri amesema serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na President Dr. John Pombe Magufuli imedhamiria kutatua kero zote zisizo rafiki kwa wananchi kwa utekelezaji wa mkataba wa wananchi na CCM kupitia ilani ya uchaguzi ya mwaka 2015-2020.
Amewafikishia wakazi wa Arusha salamu za JPM kuwa anahitaji ushindi wa kishindo wa zaidi ya kura 12,000 na hiyo itakuwa zawadi pekee kwake.
“Ndugu zangu sisi wana CCM tunaweza kujadiliana harusi itafungwa vipi na wapi, tunaweza tukajadiliana aina ya magari ya kununua lakini hatuwezi kuwa na mjadala wa namna yoyote ile kwenye utafutaji wa dola ni lazima CCM ishinde” -Kheri James
Share:

DIAMOND NA HARMONIZE WADHIHIRISHIA UMMA UJIO WA REDIO YAO

Baada ya kutuonesha mjengo mpya ambapo ndio zitakuwa ofisi za radio ya Wasafi FM na Wasafi Tv  sasa CEO wa WCB Diamond Platnumz  leo January 12, 2018 amepost picha inayomuonesha yuko na Harmonize huku nyuma yao kukiwa na mnara mrefu ambao inawezekana ukawa ndiyo mnara wa radio tuliyo ahidiwa..
Diamond amepost picha hiyo na kuandika Caption iliyosomeka…What a Busy Day #Mnarani…. InshaAllah Mwenyez Mungu atujaalie sisi Pamoja nawe Mwaka 2018 Uwe Mwaka Mwema na Wamafanikio…Tuseme “Ameen” Cc @harmonize_tz” – Diamond

Huwenda huu ukawa ndiyo mnara wa radio aliyoahidi kuileta kwa mashabiki wake na inategema kukamilika mwezi February mwaka huu 2018..
Share:

Tuesday 28 November 2017

BEYONCE 'NDANI' HARUSI YA BALE

Gareth Bale na mpenzi wake.
NYOTA wa soka wa klabu ya Real Madrid ya Hispania na timu ya taifa ya Wales, Uingereza, Gareth Bale, ameripotiwa kumtaka staa wa muziki Mmarekani, Beyonce, kutumbuiza siku ya harusi yake mwaka kesho.
Hata hivyo, itambidi Bale zimtoke Paundi milioni l.5 (Sh. bilioni 4.4) ili kupata burudani ya nyota huyo maarufu duniani.
Bale anategemea kumwoa mpenzi wake wa siku nyingi, Emma Rhys-Jones, ambapo anataka mwanamuziki huyo wa kundi lililokuwa linajulikana kama Destiny’s Child, awaburudishe waalikwa.
Beyonce.
Ndoa hiyo iliyotakiwa kufanyika nchini Italia mapema, ilichelewa kutokana na baba wa Rhys-Jones kufungwa kutokana na utapeli nchini Marekani.
Wawili hao wamefahamiana tangu utotoni na wanaishi jijini Madrid na watoto wao wa kike wawili. Baada ya sherehe hiyo huko Italia, wamepanga kufanya sherehe nyingine huko Wales.
Bale ana mkataba na Real Madrid ambapo analipwa Sh. milioni 894 kwa wiki (Paundi 300,000) na anasemekana anaweza kuhama kwenda Manchester United ya Uingereza. Beyonce, aliyeoana na nyota wa muziki wa hip-hop, Jay-Z mwaka 2008, ameuza rekodi zipatazo milioni 100 akiwa msanii anayejitegemea.
Share:

Huu ndiyo mshahara anaopewa Mugabe kwa mwezi


Robert Mugabe alijiuzulu Novemba 21 baada ya kuahidiwa kinga ya kutoshtakiwa, kulipwa dola za Marekani 10 milioni kwa mkupuo, mshahara wa kila mwezi, matibabu, usalama wake pamoja na ulinzi wa mali zake, gazeti la Independent limeandika.


Uchunguzi uliofanywa na Independent umefichua kwamba watu wa Mugabe walioshiriki katika mazungumzo yaliyowezesha yeye kuondoka walifanikiwa kufikia makubaliano na majenerali kuhakikisha mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 93 haendi kuishi uhamishoni bali afurahie kustaafu kwake nchini Zimbabwe na apate marupurupu yake.

“Serikali itamlipa Mugabe dola 5 milioni kwa mkupuo na kisha kiasi kinachosalia atakuwa akilipwa kwa mafungu,” chanzo kimoja kimesema. “Mugabe atapatiwa matibabu pamoja na mshahara kamili kila mwezi. Na ikiwa atafariki mkewe atakuwa analipwa nusu mshahara kila mwezi.”

Mugabe alifanya majadiliano ili aweze kuondoka salama kupitia timu ya wapatanishi ambayo ilijumuisha kasisi wa Kikatoliki, Fidelis Mukonori na gavana wa zamani wa RBZ Gideon Gono. Mukonori alisema katika mahojiano kwamba wajibu wake ulikuwa kuwa mpatanishi kati ya majenerali na Mugabe.
Share:

Trioni 1.8 kumuondoa Mess Barcelona


Mshambuliaji wa FC Barcelona ambaye pia ni nahodha wa timu ya taifa ya Argentina Lionel Messi hivi karibuni ameripotiwa kuamua kuongeza mkataba mpya wa kuendelea kusalia FC Barcelona.

Barcelona ni timu ambayo imemlea Lionel Messi toka akiwa katika kituo cha kukuzia vipaji cha Barcelona kinachojulikana kwa jina la La Masia.

Messi ameamua kuongeza mkataba mpya na FC Barcelona utakaomuweka Nou Camp hadi mwaka 2021 kubwa lililochukua headlines katika mkataba wa Lionel na kuzua mijadala ni kipengele kilichopo katika mkataba wake, kama kuna club itakayofikiria kumuondoa Lionel Messi FC Barcelona kama PSG walivyofanya kwa Neymar.

Watahitaji kutoa dau la pound milioni 626 ambazo ni zaidi ya Tsh Trioni 1.8, Lionel Messi hadi anasaini mkataba mpya wa kuendelea kuitumikia FC Barcelona, alikuwa ameichezea game 602, akifunga jumla ya magoli 523 na ametwaa mataji 30 akiwa na FC Barcelona na bado historia inaendelea hadi 2021.
Share:

Monday 13 November 2017

MWALIMU ATUPWA JELA KWA KOSA LA KUMTUMIA PICHA ZA UTUPU MWANAFUNZI WAKE

Mwalimu wa somo la Mapishi katika shule ya Sekondari ya St. Charles High School mjini Maryland nchini Marekani amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela kwa kosa la kumtongoza na kumtumia picha za utupu mwanafunzi wake wa kiume mwenye umri wa miaka 17.

Kwa mujibu wa maelezo kutoka kwenye mtandao wa kituo cha runinga cha  Fox 5 DC Mwalimu huyo aliyetambulika kwa jina la LaToya Nicole Parker (40) imeelezwa kuwa alikuwa anamtuma mwanafunzi huyo kwenye supermarket kipindi cha mapumziko na kwenda nae nyumbani kwake.

Kisa hicho ambacho kiliripotiwa na wazazi wa mwanafunzi huyo mwezi machi mwaka huu, 2017 kwenye kituo cha polisi kabla ya kupelekwa mahakamani ambapo mshtakiwa alikiri kutenda kosa hilo jumatatu ya wiki iliyopita.

Upelelezi uliofanywa na polisi pamoja na ushahidi uliotolewa mahakamani unaonesha kuwa mwalimu huyo alianza kumtongoza mwanafunzi huyo tangu mwezi April mwaka huu , 2017 kwa kumuandikia barua za mahaba, kumtumia picha zake za utupu na kumuahidi pesa mwanafunzi huyo kama angelikubali.

Kwa upande mwingine mwalimu mkuu wa shule ya St. Charles High School Principal, Richard Conley amesema mwalimu huyo alikuwa anafundisha somo la Mapishi shuleni hapo na alikuwa hajaajiriwa rasmi shuleni hapo bali alikuwa anafanya kazi kwa muda (Temporary) tangu mwezi Machi mwaka huu 2017.

“Baada ya kupata malalamiko kutoka kwa wazazi wake mapema tulimsimamisha kazi Ms. Parker kwani tayari walikuwa wameshatoa taarifa polisi ili kupisha uchunguzi.“amesema Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Richard Conley.

Polisi mjini Maryland wamesema walikuta picha 5o za utupu za mwalimu huyo na jumbe 303 zilizotumwa kwenye simu ya mwanafunzi huyo nyingi zikiwa za mahaba.

Mahakama mjini Maryland inayoshughulikia kesi za watoto imetoa hukumu kwa mwalimu huyo kwenda jela mwaka mmoja au kulipa faini ya dola $20,000 sawa na Tsh milioni 44 kwa kosa la kusambaza picha za utupu kwa watoto na udhalilishaji.
Share:

POLE YA MAKONDA KWA LULU YAZUA MTAFARUKU

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda,  leo ameposti kupitia account yake ya Instagram ujumbe wa kumpa moyo mwigizaji wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’ baada ya Mahakama Kuu kumhukumu kwenda jela kwa miaka miwili  kwa kumuua mwigizaji Steven Kanumba.
Ujumbe huo ulikuwa na maneno: There is a room in every situation. Stay strong, Dady is coming! yakimaanisha kwamba kuna nafasi katika kila hali.  Endelea kujipa moyo, Baba anakuja!
Mkuu wa mkoa huyo hakufafanua wazi aliposema Baba, akimaanisha Baba Mungu au Baba yupi.
Share:

Ads

Blog Archive