Friday 12 January 2018

UVCCM: INAWEZEKANA TUSIFANYE KAMPENI 2020

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Taifa, Kheri James amesema kuwa CCM haina sababu ya kufanya kampeni katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 badala yake kuna kila sababu ya kupita bila kupingwa kutokana na uimara wa CCM na serikali yake.
 Kheri ameyasema hayo wakati akizungumza na timu mbalimbali za kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani wa Kata ya Kimandolu mkoani Arusha kutoka jumuiya za CCM.
 Kheri amesema serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na President Dr. John Pombe Magufuli imedhamiria kutatua kero zote zisizo rafiki kwa wananchi kwa utekelezaji wa mkataba wa wananchi na CCM kupitia ilani ya uchaguzi ya mwaka 2015-2020.
Amewafikishia wakazi wa Arusha salamu za JPM kuwa anahitaji ushindi wa kishindo wa zaidi ya kura 12,000 na hiyo itakuwa zawadi pekee kwake.
“Ndugu zangu sisi wana CCM tunaweza kujadiliana harusi itafungwa vipi na wapi, tunaweza tukajadiliana aina ya magari ya kununua lakini hatuwezi kuwa na mjadala wa namna yoyote ile kwenye utafutaji wa dola ni lazima CCM ishinde” -Kheri James
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive