Ikiwa ni siku chache baada ya uongozi wa Yanga kumsajili Papy Tshishimbi, raia wa DR Congo, zengwe limeibuka.
Wakala
wa aliyekuwa kiungo wa timu hiyo, Justine Zulu ‘Mkata Umeme’, Karin Nir
raia wa Israel amepanga kupeleka mkataba wa mteja wake huyo katika
Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF), leo, lengo lake likiwa ni kuzuia
Yanga kuendelea kumtumia.
Tshishimbi ndiye amechukua nafasi ya Zulu raia wa Zambia ameshindwana na Yanga.
Novemba,
mwaka jana, Yanga iliingia mkataba wa mwaka mmoja na Zulu mbele ya
wakala wake huyo raia wa Israel, lakini hivi karibuni ilitangaza
kuachana na kiungo huyo kutokana na kiwango chake kutowaridhisha ambapo
nafasi yake imechukuliwa na Tshishimbi.
Hata
hivyo, wakala wa Zullu amesisitiza mkataba wa mteja wake umevunjwa
kiholela, hivyo kitendo cha jina lake kung’olewa Yanga na nafasi yake
kuchukuliwa na Tshishimbi ni haramu.
Awali,
Mkata Umeme inadaiwa alipanga kuishitaki Yanga katika Shirikisho la
Soka la Kimataifa (Fifa) ili alipwe dola 100,000 (Sh milioni 221) endapo
Yanga ingekataa kumrejesha kwenye timu hiyo kutokana na mkataba
walioingia.
Wakala
wa mchezaji huyo, tayari yupo hapa nchini tangu Ijumaa ya wiki
iliyopita alipotua akitokea kwao Israel kwa ajili ya kulimaliza suala
hilo lakini anadai viongozi wa Yanga wamekuwa wakigoma kupokea simu yake
kwa lengo la kumalizana kwa amani hali linayomlazimu kuchukua maamuzi
makubwa zaidi.
Nir amesema: “Yanga wamekatisha mkataba na mteja wangu kwa ujanjaujanja kitu
ambacho hakipo kisheria lakini pia hawataki tumalizane kwa usalama,
hawataki kupokea simu yangu licha ya kuwa nipo hapa tangu Ijumaa, kesho
(leo Jumatatu) nitakwenda TFF kupeleka mkataba wa Zullu ambao haujaisha
maana najua sheria za hapa zinaruhusu wachezaji saba pekee wa kimataifa
ndani ya timu moja.
“Najua
wamemsajili mchezaji kutoka DR Congo kitu ambacho ni kinyume cha sheria
kwa sababu Zulu mkataba haujaisha na nitaupeleka TFF ili kuona
Yanga ilivyowadanganya kwani katika mfumo wa TMS bado inaonyesha ni
mchezaji wao, baada ya hapo nadhani Simba na Azam wataenda kulalamika
TFF kwa kitendo cha Yanga kusajili wachezaji nane ili wakatwe pointi,”
alisema Nir.
Ikumbukwe Yanga ilishatangaza kuachana na mchezaji huyo kwa kukatisha mkataba wake wa mwaka mmoja.
0 comments:
Post a Comment