Tuesday 5 September 2017

BAADA YA MAHAKAMA KUMKABIDHI MANJI POLISI HIKI NDIYO KIMETOKEA

Aliyekuwa Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Yusuph Manji, akiongozana na polisi
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam leo limemkabidhi mfanyabiashara, Yusuf Manji na wenzake kwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya kumaliza upelelezi wao wa kumhoji katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili yeye na wenzake.
Akizungumza wakati wa kesi hiyo,  Wakili wa Serikali, Mutalemwa Kishenyi, amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi,  kuwa washtakiwa hao wamerudishwa tena Mahakamani ilivyokuwa imeamuru warudishwe baada ya Polisi kumaliza mahojiano yao.
Naye, Hakimu Shaidi alisema kesi hiyo itaendelea na utaratibu kama ilivyokuwa mwanzo na hivyo ameahirisha kesi hiyo hadi Septemba 8, mwaka huu.
Jana Mahakama hiyo iliruhusu Yusuf Manji na wenzake watatu kwenda kuhojiwa na Polisi kwa lengo la kukamilisha upelelezi wa kesi hiyo.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive