Tuesday 28 November 2017

BEYONCE 'NDANI' HARUSI YA BALE

Gareth Bale na mpenzi wake.
NYOTA wa soka wa klabu ya Real Madrid ya Hispania na timu ya taifa ya Wales, Uingereza, Gareth Bale, ameripotiwa kumtaka staa wa muziki Mmarekani, Beyonce, kutumbuiza siku ya harusi yake mwaka kesho.
Hata hivyo, itambidi Bale zimtoke Paundi milioni l.5 (Sh. bilioni 4.4) ili kupata burudani ya nyota huyo maarufu duniani.
Bale anategemea kumwoa mpenzi wake wa siku nyingi, Emma Rhys-Jones, ambapo anataka mwanamuziki huyo wa kundi lililokuwa linajulikana kama Destiny’s Child, awaburudishe waalikwa.
Beyonce.
Ndoa hiyo iliyotakiwa kufanyika nchini Italia mapema, ilichelewa kutokana na baba wa Rhys-Jones kufungwa kutokana na utapeli nchini Marekani.
Wawili hao wamefahamiana tangu utotoni na wanaishi jijini Madrid na watoto wao wa kike wawili. Baada ya sherehe hiyo huko Italia, wamepanga kufanya sherehe nyingine huko Wales.
Bale ana mkataba na Real Madrid ambapo analipwa Sh. milioni 894 kwa wiki (Paundi 300,000) na anasemekana anaweza kuhama kwenda Manchester United ya Uingereza. Beyonce, aliyeoana na nyota wa muziki wa hip-hop, Jay-Z mwaka 2008, ameuza rekodi zipatazo milioni 100 akiwa msanii anayejitegemea.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive