Sunday 27 August 2017

NYONI AMFUATA KAPOMBE

 
Beki mpya wa Simba, Erasto Nyoni ameanza kufuata nyayo za beki mwingine wa timu hiyo, Shomari Kapombe katika kutupia mabao.
Kapombe ndiye beki alifunga mabao mengi katika miaka ya karibuni ambapo alifunga mabao manane Ligi Kuu msimu wa 2015/16.
Hata hivyo Nyoni ambaye ametua Simba msimu huu, ameanza kuweka rekodi ya aina yake baada ya kufunga mabao manne katika mechi nane alizocheza hivi karibuni.
Nyoni alianza kwa kufunga bao safi kwenye mchezo wa Taifa Stars na Zambia katika michuano ya COSAFA kabla ya kufunga tena katika mchezo wa kirafiki kati ya Bidvest Wits ya Afrika Kusini na Simba.
Beki huyo anayemudu kucheza nafasi zote za ulinzi, alifunga pia dhidi ya Gulioni ya Zanzibar kabla ya kufunga tena dhidi ya Ruvu Shooting juzi Jumamosi hivyo kuwa beki wa Simba aliyecheka na nyavu
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive