Friday 22 September 2017

PIGO WANAWAKE WAPOTEZA ALAMA KWENYE LISTI YA MATAJIRI DUNIANI


Mwanamke anayetajwa kuwa tajiri zaidi duniani ambaye na mrithi wa Kampuni ya L’Oreal Ufaransa, Liliane Betterncourt amefariki dunia akiwa na miaka 94.
Liliane ambaye utajiri wake ulitajwa na jarida Forbes na Orodha ya Matajiri Duniani (Bloomberg Billionaire Index) kuwa ni wa Dola za Marekani bilioni 44 sawa na Shilingi trilioni 105.6, amefariki nyumbani kwake lakini kumekua na habari kwamba mwanamama huyu alikua na tatizo la akili.
Akiwa na umri wa miaka 15 Liliane alijiunga na kampuni ya baba yake ya L’Oreal ambayo ilijishughulisha na vipodozi ili kujifunza kuendesha biashara hiyo na mwaka 1957 akiwa na 24 alirithi rasmi kampuni hiyo ya baba yake ambayo aliiendesha mpaka alipoiacha akiwa na miaka 89 mwaka 2012 kutokana na matatizo hayo ya kiafya.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive