Tshishimbi
ni usajili mpya lakini katika soko la jezi, yeye ndio anaongoza kwa
jezi hiyo namba 24 akipambana na Mnyarwanda Haruna Niyonzima aliyejiunga
na Simba na kukabidhiwa jezi namba nane.
Mwanaspoti
imeshuhudia uuzwaji wa jezi sehemu mbalimbali kama Kariakoo, Manzese na
stendi ya mabasi yanayokwenda mikoani Ubungo jijini Dar es Salaam.
Muuzaji
wa jezi hizo nje ya stendi ya mabasi Ubungo, Issa alisema: “Biashara ya
jezi ni nzuri kwa kipindi hiki cha maandalizi ya mechi ya Simba na
Yanga, na safari hii jezi inayouzika kwa wingi ni ya Tshishimbi anamzidi
kidogo Niyonzima”
“Jezi hizi zina vipindi, mwanzoni
kipindi cha usajili kilipoanza, Shiza Kichuya kwa Simba na Ibrahim Ajibu
kwa Yanga walikuwa juu, kisha Niyonzima alipojiunga Simba akashika soko
kwa kiasi na sasa Tshishimbi ni kama wanachuana.”
0 comments:
Post a Comment