Wednesday, 2 November 2016

MADINI MAPYA YAGUNDULIWA TANZANIA


Tanzanite ni madini yanayopatikana Tanzania pekee; madini haya yameipaisha Tanzania duniani kote na kukuza uchumi wake. Wakati nchi hiyo ikiwa na madini lukuki ya kila aina leo madini mapya yamegunduliwa katika eneo lenye madini ya kipekee la Manyara na kupewa jina Merelaniite.

Jina hilo limetokana na eneo ambalo madini hayo yalipatikana, Merelani (Mererani) katika milima ya Lelatema katika Wilaya ya Simanjiro huko mkoani Manyara.Madini hayo yamegunduliwa na wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Kiteknolojia cha Michigan cha Marekani, makavazi ya historia asilia ya London, Chuo Kikuu cha Di Firenze cha Italia na makavazi ya historia asilia ya Smithsonian ya Washington.

Wataalamu sita waliofanya uchunguzi, kwenye makala iliyochapishwa kwenye jarida la Minerals (Madini) wanasema madini hayo yana vipande vinavyofanana na sharubu vya rangi ya kijivu vya urefu wa milimita moja, ingawa kuna baadhi vyenye urefu wa hadi mililita 12.

Madini hayo yanakaribiana na madini ya zoisite (aina ya tanzanite), prehnite, stilbite, chabazite, tremolite, diopside, quartz, calcite, graphite, alabandite na wurtzite.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive