Wednesday, 2 November 2016

CLOUDS YAMGARAGAZA LADY JAYDEE MAHAKAMANI



Baada ya kimya cha muda mrefu hatimaye Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, imetoa hukumu ya kesi iliyofunguliwa na Clouds Media Group dhidi ya Mwanamziki mashuhuri hapa nchini Judith  Wambura akifahamika zaidi kama Lady Jaydee.kusaga_ruge 

Itakumbukwa Kampuni ya Clouds Media Group yenye vituo vya redio na tv zenye ushawishi mkubwa kwa jamii hapa nchini kupitia kwa Mkurugenzi wake Joseph Kusaga pamoja na Mkurugenzi wa vipindi na uzalishaji, Ruge Mutahaba walifungua kesi katika mahakama hiyo wakimtuhumu msanii huyo kuwachafua kupitia blog yake.

Akitoa hukumu hiyo mahakamani hapo hii leo Hakimu Boni Lyamike amemwamuru Lady Jaydee ambaye alikuwa shahidi pekee katika kesi hiyo kuwaomba radhi wakurugenzi hao kupitia vyombo vya habari kwa kuchafua taswira zao huku akitakiwa kuwalipa fidia kutokana na madhara walioyapata kwa kitendo alichowafanyia ikiwa ni pamoja na kulipa gharama za wanasheria zilizotumiwa na Clouds Media Group kwenye kesi hiyo.jaydee 

Hata hivyo msanii huyo amekiri kuandika maneno hayo ya kuwachafua mahasimu wake huku Meneja wake Seven Mosha akinukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari akisema Jaydee atazungumzia hukumu hiyo muda wowote ingawa kupitia ukurasa wake wa Instagram Jide ameandika “Iam not afraid God is with me all the time”.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive