Wednesday, 2 November 2016

WANANCHI WATAKIWA KUVUNA MAJI YA MVUA

Denis Massawe

Waziri wa Maji na Umwagiliaji Eng. Gerson Lwenge amezitaka wilaya zote nchini kujenga mabwawa ya kuvuna maji ya mvua ili kukidhi mahitaji ya maji hasa nyakati za ukame na kuwezesha kilimo cha umwagiliaji katika maeneo yao.lwengeAkizungumza na waandishi wa habari hii leo jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Wadhibiti wa Huduma za Maji Kusini na Mashariki mwa Afrika (ESAWAS), Eng. Gerson Lwenge amesema Mabwawa hayo yatasaidia kupatikana maji hasa vipindi vya ukame na maeneo ya vijijini ambako hakuna miundombinu ya maji safi na salama.wadau-ewuraNaye Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Mhandisi Mbogo Futakamba amebainisha kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imewekeza kwa kiwango kikubwa kwenye sekta ya maji ambapo mpaka sasa imekwishakamilisha ujenzi wa mtambo wa maji wa Ruvu chini unaosambaza zaidi ya lita za maji  milioni 200 kwenye Mkoa wa Dar es Salaam.mkurugenzi-ewura-felixKwa upande wa Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Felix Ngamlagosi amesema kuwepo kwa vyombo vya udhibiti wa huduma za maji kama vile ESAWAS vitasaidia kuondoa migogoro kati ya watumia maji na watoa huduma za maji.

Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive