Wednesday, 2 November 2016

RASMI JOSHUA NA KLITSCHKO KUZICHAPA MWAKANI

Denis Massawe

Pambano la ngumi kuwania ubingwa wa dunia wa uzito wa juu linalotambuliwa na WBA lililotarajiwa kupigwa Desemba 10 ndani ya Manchester Arena liliahirishwa baada ya Wladimir Klitschko kuwa majeruhi akisumbuliwa na kiazi cha mguu.Anthony Joshua

Baada ya kuarishwa kwa pambano hilo, Shirikisho la masumbwi duniani WBA limethibitisha kuwepo kwa pambano hilo mwakani kati ya mwezi Machi na April huku Joshua akipata kibali cha kupigana na Eric Molina mwezi Desemba.skysports-anthony-joshua-eric-molina-tale-of-tape_3821832Promota wa Klitschko Bernd Boente ameeleza kuwa yeye na timu nzima ya Klitschko wamefurahishwa na maamuzi ya WBA ambayo yamezingatia afya ya bondia wao.anthony-joshua

 Klitschko ambaye ni bingwa wa zamani wa dunia amepigana mapambano 68 akishinda 64 na kupoteza 4 huku 53 akishinda kwa KO. Anthony Joshua mwenye miaka 27 hadi sasa ameshapigana mapambano 17 ya uzani wa juu na kushinda yote kwa KO.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive