Wednesday 16 August 2017

KAULI YA SERIKALI KUHUSU MOTO ULIOTEKETEZA SOKA LA SIDO

Moto ulivyoteketeza Soko la Sido, Mbeya.
Natoa pole kwa wote walioathirika na janga la moto kwa wafanyabiashara soko la Sido. Soko la Sido lilianza kuungua saa 21.32 Hrs jana usiku na kuteketeza mali za wafanyabiashara wa soko la sido.
Pamoja na kutoa pole niwashukuru wananchi, vyombo vya ulinzi kwa ushirikiano na kazi kubwa ya kudhibiti moto usiendelee kuleta madhara makubwa zaidi.
Serikali kupitia Mkuu wa wilaya ya Mbeya imeunda kamati  ya kufanya tathmini ya kujua hasara na chanzo cha Moto huo .
Tunaomba wananchi waendelee kuwa watulivu na watoe ushirikiano kwa kamati hiyo ili tuweze kujua chanzo cha moto na hasara iliyopatikana
Aidha vyombo vya ulinzi vinaendelea kuchunguza kujua kama moto huo utakuwa umesababishwa na mtu/watu uchunguzi huo bado unaendelea
Nirudie tena kuwapa pole wote walioathirika na janga na Mungu awatie nguvu katika kipindi hiki kigumu
Amos G.Makalla Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive