Friday 23 June 2017

USHABIKI SAWA NA KUNYWA SUMU

 
    Shabiki wa klabu ya Yanga akibebwa na msalaba mwekundu baada ya        kupoteza fahamu.
Miongoni mwa mambo yenye uwezo mkubwa wa kuleta furaha ama huzuni iliopitiliza katika maisha ni ushabiki wa kupitiliza wa mchezo wa mpira wa miguu.
Na hili limejizidhirisha baada mkazi mmoja wa mtaa wa Mianzini, Mbagala, jijini Dar es Salaam Mzee Njimbwi kufariki dunia Jumapili iliyopita.
Sababu inayosadikika kuchukua uhai wake ni furaha aliyokuwa nayo baada ya timu ya Dar Young African maarufu Yanga, kunyakua ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Mbeya City uliyoifanya Klabu ya Yanga kufikisha pointi 65 sawa na mahasimu wao Simba Spot Club huku ikiongoza ligi kwa wastani wa magoli ya kufunga na kufungwa.
Yanga ilianza kupata goli la kwanza dakika ya Saba kipindi cha kwanza mfungaji akiwa ni Simon Msuva, ambaye aliunganisha kwa kichwa mpira wa krosi uliopigwa na Hassan Hamisi Ramadhani ‘Kessy’.
Mbeya City walisawazisha goli hilo dakika ya 58 kupitia Haruna Shamte, baada ya kazi kubwa kufanywa na Ditram Nchimbi, kisha Shamte kutumbukiza mpira huo nyavuni.
Obrey Chirwa ndiye aliyeipatia timu ya Yanga ushindi, baada ya kuunganisha kwa kichwa mpira wa adhabu ndogo uliopigwa na Juma Abdul.
Ushindi huo wa klabu ya Yanga ulimfanya mzee Njimbwa kushindwa kuvumilia furaha yake wakati akiwasimulia washabiki wenzake kijiweni siku ya Jumapili Asubuhi, hivyo wenzake waliokuwa nae walishangaa kumuona mzee huyo akidondoka chini na kufariki papo hapo.
Kufuatia kifo hicho cha mzee Njimbwa kinadhihirisha kabisa jinsi ushabiki wa mchezo wa mpira unavyoshabihiana na sumu tena ya panya kwani ili lidhihirike hili, jaribu kuwa shabiki wa mpira halafu timu yako ishindwe ndo utajua ukweli wa tukio hili.

  mashabiki wa Yanga wakiwawamepoteza fahamu
Maumivu yatokanayo na ushibiki ndiyo yaliyoondoa uhai wa mzee Njimbwa  ama waulize mashabiki wa simba au Arsenal watakuelezea vizuri sana.
Mzee Njimbwa anamfuata Mkenya, Suleiman Alphonso  Omondi,  aliyejinyonga miaka sita iliyopita baada ya Arsenal kutolewa nje ya michuano ya klabu bingwa za Ulaya (Champions League), kwa kudundwa mabao 4-1 na wapinzani wao wa kijadi Manchester United.
Uadui kati ya Arsenal na Manchester United ulianza toka mwaka 1919 na ukalipuka upya miaka ya 1990, wakati wa meneja Alex Ferguson na Arsene Wenger na umahiri wa manahodha wa klabu hizo Roy Keane (Man U) na Patrick Vieira (Arsenal).
Kipindi Arsenal ikiwika kati ya mwaka 2000 na 2005, kiasi cha kuitwa ‘Invisibles’ ambapo mwaka  2003- 2004 ilimaliza ligi nzima bila kufungwa na timu yeyote.
Sasa mwaka 2009, Mkenya Omondi alighadhabika aliposhuhudia Arsenal ikimwagiwa pilipili machoni katika fainali hizo, waliomshuhudia dakika za mwisho wanasema baada ya kubaini  Arsenal imetolewa, hayati Omondi alitoka nje ya Bar ya Bamba, Embakasi, Nairobi,  akitokwa machozi.
Kesho yake maiti ya kijana huyo mwenye umri wa miaka 29 ilikutwa ikining’inia barazani, masikini Omondi alijiua akiwa amevaa jezi ya Arsenal.
Kifo ni miongoni mwa matokeo ya ushabiki uliopiliza na kama ushabiki ukikukosa kwenye kifo basi hupelekea kuwa chizi ama mwendawazimu kabisa si wa kuokota makopo bali wa kimpira yaani kufanya vitu ambavyo kitafsiri vinaonesha kuwa umependa mpaka umeloweya.

 




Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive