Utafiti umeonesha kuwa wanawake wengi waliofanyiwa upasuaji au wakati wa kujifungua hupunguza mawimbi ya maumivu yatokayo kwenye ubongo kwenda kwenye mwili iwapo walishikwa mikono na waume zao.
Dr Pavel Goldstein, akielezea hali hiyo inavyoweza kutokea kisayansi amesema cingulate cortex ambayo ni sehemu ya ubongo huchelewa kutuma taarifa kwenye ubongo kuhusu kuwepo kwa maumivu kutokana na uwepo wa homoni ya Oxytocin inayozalishwa iwapo mtu atashikana mikono na mtu wanayependana.
Utafiti pia umeonesha moyo hupungua mapigo na kuwa ya kawaida wakati wa maumivu makali kutokana na saikolojia ya binadamu kujisikia amani anapokuwa na mtu anayempenda wakati wa kuumwa. Hivyo, imeonekana ni muhimu kwa wanaume kuwashika mikono wake zao wakati wa kujifungua.
0 comments:
Post a Comment