Monday 31 July 2017

NYUMBA KUBWA ZA MABILIONEA ULAYA AKIWEMO BILL GATES


Uwezo wa watu kuishi unategemea namna ya utajiri au uwezo wa kifedha waliokuwa nao. Wanavyoingiza fedha zaidi ndivyo wanavyozidi kubalika katika namna ya kuishi. Wapo matajiri ambao hujenga nyumba ambayo kutokana na ukubwa wake inaweza kuishi hadi watu 100 na huwatumia wabunifu wa hali ya juu…
Hii hapa Top Ten ya nyumba ghali zaidi za Mabilionea
10: 360 Mountain Home Road
Nyumba hii ipo Westside, California, Marekani na inamilikiwa na Masayoshi Son, CEO wa Softbank. Kasri hili limejengwa kwa namna yake likiwa na bwawa na kuogelea la futi 1.117, uwanja wa tennis, Maktaba. Kwa sasa linakadiriwa kuwa na thamani ya Dollar Milioni 117.5 zaidi ya Tsh. Bilioni 258.

9: Xanadu 2.0
Hii inapatikana Seattle, Washington na inamilikiwa na Bill Gates, mwasisi-mwenza na Mwenyekiti wa Microsoft. Lina eneo la futi 66,000 likisanifiwa kwa mtindo wa Pacific lodge
lina maktaba binafsi, chumba cha chakula, bwawa la kuogelea ambalo lina mfumo wa muziki chini (swimming pool with underwater music system). Linakadiriwa kuwa na thamani ya Dollar Milioni 120.5 zaidi ya Bilioni 264.

8: Blossom Estate
Ukitembelea Palm Beach, Florida, utakutana na kasri hili ambalo linamilikiwa na Kenneth Griffin, Mwasisi na CEO wa Citadel LLC. Jengo kwenye ekari 8 ambalo linajumuisha nyumba nne zinazojitegemea katika eneo ambapo tatu kati ya hizo zinaangalia ufukwe. Lina thamani ya Dollar Milioni 130 zaidi ya Tsh. Bilioni 286.

7: Ellison Estate
Jumba hili linapatikana Woodside, California, ni milki ya Tajiri namba tatu katika nchi ya Marekani, Larry Ellison, mwasisi-mwenza wa Oracle Corporation. Kuna majengo 10 ndani ya ekari 23, bwawa la samaki, Ziwa lililotengenezwa, chumba cha chai, na nyumba ya bafu ambayo imesanifiwa kwa mtindo wa Kijaan. Thamani yake ni Dollar Milioni 200 zaidi ya Tsh Bilioni 440.

6: One Hyde Park
Nyumba ya ukubwa wa futi 25,000 ambayo ipo katika jiji la London, inamilikiwa na tajiri wa Ukraine, Rinat Akhtemov. One Hyde Park ni moja kati ya makazi maarufu sana United Kingdom. Thamani yake ni Dollar Milioni 213 zaidi ya Tsh. Bilioni 468.

5: 18-19 Kensington Palace Gardens
Nayo pia iko katika jiji la London, ikimilikiwa na Lakshmi Mittal, mmilikiwa wa viwanda vya kutengeneza chuma wa India. Ina vyumba 12 vya kulala, bafu la Kituruki, eneo la kuegesha magari zaidi ya 20. Wakati wa kununuliwa ilikuwa ndiyo nyumba iliyouzwa kwa bei ya juu zaidi Duniani. Awali lilimilikiwa na Berne Ecclestone, Mkuu wa Formula One ambapo thamani yake kwa sasa ni Dollar Milioni 222 ambazo ni zaidi ya Tsh. Bilioni 488.

4: Four Fairfield Pond
Hii ipo Sagaponack, New York na inamilikiwa na Ira Rennert, mwekezaji wa Marekani na Mfanyabiashara. Jumba hili lina vyumba 29 vya kulala, mabafu 39, na mabwawa 3 ya kuogelea na umeme wa kijitegemea. Thamani yake ni Dollar Milioni 248.5 zaidi ya Tsh. Bilioni 545.

3: Villa Leopolda
Kasri hili lipo Villefranche-sur-Mer, Ufaransa, likienea katika eneo la ukubwa wa ekari 18 na lilitumika kama makazi ya King Leopold II wa Ubelgiji lakini sasa linamilikiwa na Mbarazil Lily Safra ambaye amerithi baada ya kifo cha mumewe Edmond Safra. Thamani yake ni Dollar Milioni 750 zaidi ya Tsh. Trilioni 1.65.

2: Antillia
Linajulikana pia kama ‘One Billion Dollar home’, lipo katika eneo la ukubwa wa square foot 400,000 katika mji wa Mumbai, India na linamilikiwa na Bilionea Mukesh Ambani. Kutokana na ukubwa wake linahitaji watu 600 kulihudumia. Kama linavyoitwa jumba hili lina thamani ya Dollar Bilioni 1 zaidi ya Tsh. Trilioni 2.2.

1: Buckingham Palace
Kasri linamilikiwa na familia ya kifalme na kwa sasa lina thamani ya Dollar Bilioni 1.55 zaidi ya Tsh. Trilioni 3.3. kasri hili lina jumla ya vyumba 775.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive