Monday 2 October 2017

NIYONZIMA, AJIBU WAWATIBUA YANGA

Mshambuliaji wa Yanga, Ibrahim Ajibu akikabidhiwa jezi namba kumi wakati alipojiunga na klabu ya Yanga.
WAKATI kivumbi cha Ligi Kuu Bara kikizidi kupamba moto, baadhi ya mashabiki wa timu ya Simba juzi Jumamosi walijikuta wakiingia katika mvutano mkubwa na kutaka kushushiana makonde kuhusiana na mshambuliaji wa Yanga, Ibrahim Ajibu.

Mvutano huo ulitokea katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar wakati Ajibu alipokuwa akiitumikia Yanga dhidi ya Mtibwa Sugar katika mchezo uliomalizika bila ya kufungana.

Wakati mechi hiyo ikiendelea, mmoja wa mashabiki wa Simba ambaye jina lake halikuweza kujulikana, aliyekuwa uwanjani hapo akiiunga mkono Mtibwa Sugar, alidai kuwa katika usajili bora ambao Yanga wananufaika nao msimu huu ni ule wa Ajibu.
Mnyarwanda Haruna Niyonzima.
Alisema kuwa tangu ajibu ajiunge na Yanga amebadilika na sasa anacheza soka la uhakika tofauti na alivyokuwa Simba msimu uliopita na mabao yake yameweza kuisaidia Yanga kupata pointi sita lakini wao wamepata hasara kwa kumsajili, Mnyarwanda Haruna Niyonzima akitokea Yanga kwa madai kuwa hakuna chochote alichokifanya mpaka sasa tangu ajiunge na timu hiyo.

Kauli hiyo uliungwa mkono na mashabiki wengi wa Simba waliokuwa uwanjani hapo lakini ikapingwa vikali na wachache wakidai kuwa Niyonzima ni mchezaji mzuri lakini kocha wao mkuu, Mcameroon, Joseph Omog bado hajajua kumtumia, ndiyo maana anaonekana hana msaada katika timu hiyo. Hali hiyo ilizua mzozo mkubwa uliosababisha mashabiki hao kutaka kutwangana makonde. Hata hivyo, tangu Ajibu ajiunge na Yanga amefanikiwa kuifungia timu hiyo mabao mawili mpaka sasa kati na manne ambayo imefunga lakini Niyonzima hana bao lolote, ingawa yeye anacheza nafasi ya kiungo.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive