Sunday 1 October 2017

ZITTO AIBUKIA BOT

Mbunge wa Kigoma mjini Zitto Kabwe ameilalamikia benki kuu ya Tanzania kwa hatua yake ya kutokutoa taarifa za  hali ya uchumi za kila mwezi (Monthly Economic Review) kama inavyoelekezwa na sheria ya benki kuu ya mwaka 2006, Kupitia ukurasa wa Facebook wa Mbunge ameandika ujumbe huu...

"Miezi 4 Benki Kuu ( BoT ) imekalia Taarifa nyeti za Uchumi ( MER ). Kinafichwa nini?

Benki Kuu ya Tanzania inapaswa, Kwa mujibu wa Sheria ya Benki Kuu ya mwaka 2006 ikisomwa pamoja na kanuni zake, kutoa Taarifa ya kila Mwezi ya Mapitio ya Uchumi ( Monthly Economic Review). 

Tangu nianze kusoma Taarifa hizi nikiwa Chuo Kikuu hii ni Mara ya kwanza imepita miezi 4 MER haijachapishwa kwenye tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania. Mara ya mwisho imewekwa Taarifa ya Mwezi June inayoeleza mapitio ya mwezi Mei 2017. Taarifa hiyo ya mwisho ilionyesha kuwa mauzo yetu nje Kwa bidhaa za viwanda yameporomoka Kwa zaidi ya USD 700 milioni sawa na Bombadier mpya 21 Hivi.

Serikali ya CCM ya Awamu ya Tano ambayo imejiondoa kwenye Mpango wa kuendesha Serikali Kwa Uwazi ( OGP ) na kujipa Sifa ya kufungia magazeti kuliko Awamu yeyote tangu tupate Uhuru Sasa imeamua kutunyima na Taarifa za kisheria kabisa kuhusu Uchumi.

Kwa kuchelewa huku, Taarifa itakayotoka lazima itakuwa ya kupikwa pikwa."
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive