Sunday 1 October 2017

BAADA YA SIMBA KUILAZA STAND MANARA, MWANJALI WASEMA HAYA

Baada ya timu ya Simba kuzima kelele na vijembe vya mashabiki wa Stand United kwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 yaliyofungwa na Shiza Kichuya pamoja na Laudit Mavugo kwenye Uwanja wa Kambarage mkoani Shinyanga leo Jumapili msemaji wa timu hiyo Haji Manara atoa ya moyoni.
Ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram Msemaji huyo alituma ujumbe uliosoka hivi "Alhamdulilah, muhimu tumepata points tatu leo, Simba raha sana."
Kikosi hicho ambacho kimefanikiwa kuchomoka na pointi tatu muhimu, kimeleta matumaini kwa mashabiki wao baada ya mchezo uliopita kutoka sare ya mabao 2-2 na Mbao FC.
Timu hiyo imepanda kileleni ikiwa imefikisha pointi 11 ambazo zimefikiwa na Azam FC pamoja na Mtibwa huku watani zao Yanga walikwaa kisiki jana baada kutoka suluhu ya 0-0 dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Uhuru jana Jumamosi.
Nahodha wa timu hiyo, Mwanjali alisema wanampongeza kipa wao Aishi Manula kwa kuokoa hatari nyingi, huku akisistiza kuyafanyia kazi upungufu uliyojitokea katika kikosi hicho cha leo.
Hata hivyo aliongeza kuwa awali kikosi hicho kililala jambo ambalo liliwapa nafasi wapinzani wao kufunga bao la kufutia machozi.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive