Baada ya timu ya Simba kuzima kelele na vijembe vya mashabiki wa
Stand United kwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 yaliyofungwa na
Shiza Kichuya pamoja na Laudit Mavugo kwenye Uwanja wa Kambarage mkoani
Shinyanga leo Jumapili msemaji wa timu hiyo Haji Manara atoa ya moyoni.
Ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram Msemaji huyo alituma ujumbe uliosoka hivi "Alhamdulilah, muhimu tumepata points tatu leo, Simba raha sana."
Kikosi hicho ambacho
kimefanikiwa kuchomoka na pointi tatu muhimu, kimeleta matumaini kwa
mashabiki wao baada ya mchezo uliopita kutoka sare ya mabao 2-2 na Mbao
FC.
Timu hiyo imepanda kileleni ikiwa imefikisha pointi
11 ambazo zimefikiwa na Azam FC pamoja na Mtibwa huku watani zao Yanga
walikwaa kisiki jana baada kutoka suluhu ya 0-0 dhidi ya Mtibwa Sugar
kwenye Uwanja wa Uhuru jana Jumamosi.
Nahodha wa timu
hiyo, Mwanjali alisema wanampongeza kipa wao Aishi Manula kwa kuokoa
hatari nyingi, huku akisistiza kuyafanyia kazi upungufu uliyojitokea
katika kikosi hicho cha leo.
Hata hivyo aliongeza kuwa awali kikosi hicho kililala jambo ambalo liliwapa nafasi wapinzani wao kufunga bao la kufutia machozi.
0 comments:
Post a Comment