Saturday 30 September 2017

PEP GURDIOLA ALIVYOSHUSHA REKODI YA CHELSEA

Haikuwa siku nzuri kwa Antonio Conte na mbinu za Pep Gurdiola zilimpoteza kabisa, ilikuwa mbaya kwa Chelsea kwani ndio mchezo wa kwanza kwa Chelsea kupiga mashuti machache.
Chelsea hawajawahi kupiga mashuti yaliyolenga bao chini ya 5 tangu Conte ajiunge nao, lakini hii leo wamepiga mashuti manne tu huku kuanzia dakika ya 26 hadi mpira unaisha walipiga mashuti mawili tu.
Manchester City walipata bao lao la kwanza na la pekee kupitia kwa Kelvin De Bruyne na kuwafanya sasa kuwa wamecheza michezo minne mfululizo wakishinda bila kuruhusu bao katika Epl.
Kule nchini Ufaransa Kylian Mbappe alifunga moja ya bao katika ushindi wa bao 6 kwa 2 dhidi ya Bordeaux na kumfanya kinda huyo kuhusika katika mabao 29 ya ligi ya Ligue 1 msimu huu akifunga 14 na kuasisst 5.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive