Monday 4 September 2017

SIMBA YAIKWEPA TP MAZEMBE YAKUMBANA NA VISIKI

 
SIMBA iliyorejea katika anga za kimataifa baada ya kukaa pembeni muda mrefu, huenda ikawa na kibarua kizito katika mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika mwakani, kwani licha ya kuikwepa TP Mazembe ya DR Congo, iko mikononi mwa timu 10 vigogo Afrika.
Simba iliyotwaa tiketi ya kushiriki mashindano hayo ya CAF kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2013, italazimika kuchuana na timu hizo huku Difaa el Jadida ya Simon Msuva ikitarajiwa kuzengea kukutana na Yanga katika Ligi ya Mabingwa.
Timu ambazo tayari zimefuzu na ambazo Simba itahitaji kutumia akili ya ziada endapo itakumbana nazo ni Zamalek na El Masry kutoka Misri pamoja na Club Africans na Ben Guerdane za Tunisia.
Sio hizo tu, ipo USM Algers na CR Belouizdad za Algeria ambazo tayari zimepata tiketi ya kushiriki mashindano hayo ya pili kwa ukubwa Afrika katika ngazi ya klabu.
Timu nyingine ambayo tayari imetwaa tiketi hiyo ni Cape Town City na Super Sports United za Afrika Kusini na timu ya zamani ya Joseph Omog, AC Leopards ya Congo na Raja Casablanca ya Morocco.
Katika mashindano hayo ya CAF timu zitakazofuzu hatua ya makundi zitakuwa zimejihakikishia kupata dola 150,000 (Sh331 milioni) hadi Dola 239,000 (Sh527 milioni).
Kwa upande mwingine, watani zao Yanga watakuwa na kibarua kigumu zaidi katika Ligi ya Mabingwa Afrika kwani kuna uwezekano wakakutana na Msuva akiwa na El Jadida yake waliokata tiketi sambamba na Wydad Casablanca.
Nyingine ni Al Ahly na Misr Lel Makkasa za Misri, Esperance na Etoile Du Sahel za Tunisia, TP Mazembe na AS Vita za DR Congo, ES Setif na MC Alger iliyoitoa Yanga kwa jumla ya mabao 4-1 kwenye  play-off za Kombe la Shirikisho Afrika.
Nyingine zitazoikabili Yanga ni Mamelodi Sundowns na Bidvest Wits za Afrika Kusini, ASEC Memosas na Mbabane Swallows aliyoichezea kiungo wake mpya, Kabamba Tshishimbi.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive