Wednesday 6 September 2017

HAYA NDIYO MANENO YA MKUDE KUELEKEA MECHI YAO NA AZAM

 
Kiungo mkabaji wa Simba,Jonas Mkude amesema mechi dhidi ya Azam inahitaji akili zaidi.
Simba watakuwa wageni wa Azam, Jumamosi hii kwenye Uwanja wa Azam Complex ukiwa ni mchezo wa pili wa Ligi Kuu Bara.
"Azam  si timu ya kubeza walianza vema mechi yao na Ndanda kwa kuwafunga bao 1-0 na kujikusanyia pointi tatu na sisi tuliwafunga Ruvu Shooting kwa mabao 7-0, kila mtu ana hamu ya kuona anaendeleza furaha,"alisema Mkude.
Alisema  anaamini Simba itaibuka na ushindi mnono dhidi ya Azam kwa madai wamejipanga kuhakikisha wanaendeleza gurudumu la ushindi.
"Hakuna kazi rahisi kwani kila timu ipo kwa ajili ya kuvuna pointi tatu ndivyo ilivyo na kwetu kuona tunafika mbali na mwisho wetu uwe ubingwa,"alisema Mkude.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive