Saturday 23 September 2017

BAADA YA KUKAZIWA NA MBAO OKWI ASEMA HAYA


Mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi.

STRAIKA wa Simba, Emmanuel Okwi, amesema hakuweza kufanya vizuri katika mchezo dhidi ya Mbao FC, kwani mabeki wa wapinzani wao hao walimkamia kupita kiasi.

Okwi hakuweza kufurukuta dhidi ya Mbao FC katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa juzi Alhamisi kwani alitulizwa kwa kuchezewa rafu mara 12.

Katika mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mbao iliilazimisha Simba sare ya mabao 2-2 na kuwa timu ya kwanza kutikisa nyavu za Wekundu wa Msimbazi msimu huu.

Okwi, mwenye mabao sita katika ligi kuu akiwa kinara wa ufungaji, alishindwa kufunga kutokana na mabeki wa Mbao kuwa makini wakiongozwa na Boniface Maganga na Yusuph Mgeta.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive