Sunday 13 August 2017

RAIS MAGUFULI NA MKEWE WAUNGAUNA NA WAUMINI MISA TAKATIFU ST.JOSEPH

Rais Magufuli na Mkewe, Mama Janeth Magufuli wakagana na Askofu Mkuu wa 
Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo baada ya 
kushiriki Ibada ya Misa takatifu, Dominica ya 19 ya mwaka A wa Kanisa, katika Kanisa 
Kuu la Mtakatifu Joseph jijini Dar es Salaam leo Agosti 13, 2017.

Rais Magufuli na Mkewe,  Mama Janeth Magufuli wakitakiana amani na watawa wakati wa 
Ibada ya Misa hiyo.

Rais Magufuli akiwapungia mkono waumini baada ya kushiriki Ibada ya Misa.

Rais Magufuli akipiga picha ya kumbukumbu na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la 
Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, Padre Vicent na baadhi ya 
wanafunzi shule ya Sekondari ya St. Joseph baada ya kushiriki Ibada ya Misa hiyo.

…Wakijumuika na waumini wengine kushiriki Ibada ya Misa hiyo.

Rais Magufuli na Mama Janeth Magufuli wakiwa katika Ibada ya Misa takatifu.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Mkewe, Mama Janeth Magufuli leo wameungana na waumini wengine kushiriki Ibada ya Misa Takatifu, Dominika ya 19 ya mwaka A wa Kanisa, katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph jijini Dar es Salaam.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive