Thursday 31 August 2017

MAMADOU SAKHO THE DILL DONE

Mamadou SakhoHaki miliki ya picha
Crystal Palace wamekamilisha usajili wa beki wa Mamadou Sakho kutoka Liverpool kwa £26m.
Palace walifanikiwa baada ya kuwasilisha ombi lao la nne la kutaka kumsajili mchezaji huyo wa miaka 27.
Walikuwa wamewasilisha dau ya £25m Jumanne lakini ikakataliwa.
Liverpool awali walikuwa wamesema hawangekubali chini ya £30m kwa beki huyo wa Ufaransa, ambaye alifana sana akiwa kwa mkopo Selhurst Park msimu uliopita.
Sakho alijipata akiwa mchezaji wa ziada Anfield baada ya kutoelewana na meneja Jurgen Klopp.
Mwenyekiti wa Paris Steve Parish hatimaye alifanikiwa baada ya dau yake ya £22m na vikolezo vya £3m kukataliwa awali.
Mamadou SakhoHaki miliki ya picha
Hata baada ya kutofikisha lengo lao la £30, Liverpool bado walipata faida kutoka kwa mchezaji huyo ambaye walikuwa wamemnunua £18m kutoka Paris St-Germain Septemba2013.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive