Kocha George Lwandamina amemuambia kiungo wake mpya,
Papy Kambamba Tshishimbi kuwa ataangalia ufiti wake ili kuona kama
atampanga katika mechi ya Jumatano dhidi ya Simba.
Tshishimbi amechelewa kujiunga na kambi ya Yanga mjini Pemba, lakini tayari ameanza mazoezi mazoezi.
“Kweli kocha atakachoangalia ni fitnesi yake kwanza,
hivyo ameanza mazoezi na baada ya hapo ndiyo atajua anapaswa kumpanga au
la.
“Kama atakuwa fiti ataanza, kama hatakuwa fiti basi ni
suala la kusubiri kwa kuwa ni vizuri mchezaji kumpa nafasi akiwa fiti,”
kilieleza chanzo.
0 comments:
Post a Comment