Friday 4 August 2017

HIZI NDIYO MBWEMBWE ZA NEYMAR BAADA YA KUTUA PSG



Nyota wa soka wa Brazil, Neymar Jr ametambulishwa rasmi na klabu yake mpya ya Paris Saint-Germain (PSG) ya nchini Ufarasa baada ya kukamilisha usajili kutoka Barcelona kwa ada ya uhamisho ya Tsh 579 bilioni ambayo imevunja rekodi ya dunia.


Wakati wa mkutano na waandishi wa habari, Neymar alisema kwa muda mrefu alikuwa hajui hatma yake na kwamba, wachezaji wengi wa Brazil walikuwa wakimshawishi ajiunga na PSG.


Aidha, Neymar ambaye hakueleza sababu za kuamua kuikimbia Barcelona, amesema kwamba hajajiunga na PSG ili awe mchezaji mkubwa klabuni hapo.


Akieleza masikitiko yake, Neymar alisema kwamba bado anaiheshimu klabu ya Barcelona lakini amesikitishwa na ukosoaji uliofanywa na mashabiki huku baadhi yao wakienda mbali na kuchoma jezi zake.

Kutokana na uhamisho huo wa ghali zaidi duniani,  Neymar atalipwa mshahra baada ya makato Tsh 1.6 bilioni kwa wiki ambapo kwa mwezi atalipwa Tsh 6.4 bilioni akiitumikia PSG.


Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive