Wednesday 9 August 2017

HARUNA HAIKUMBUKA YANGA


Kiungo mpya wa Simba Haruna Niyonzima amesema haikuwa rahisi kwake kuhama kutoka Yanga kwenda Simba lakini kwa kuwa yeye ni mchezaji na hajui ataishia wapi, alichukua uamuzi wa kuondoka Yanga pale wakati ulipofika.
“Haikuwa rahisi kuhama Yanga lakini naamini kuna wana Yanga na wapenzi wa Haruna wameumia lakini mimi niseme yote ni maisha, mimi mcheza mpira siwezi kujua nitaishia wapi lakini kikubwa ni kufanya kazi yangu. Nawashukuru Yanga, kwa sababu ni timu ambayo nimecheza misimu mingi sana kuliko timu zote duniani,” Haruna Niyonzima.
Niyonzima ametambulishwa mbele ya mashabiki wa Simba siku ya Simba Day ambayo huadhimishwa na wana Simba August 8 kila mwaka.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive