Friday 14 July 2017

VENUS AMTUPA NJE JOHANNA KONTA

Venus akisherekea ushindi
Matumaini ya Muingereza Johanna Konta kufika fainali za Wimbledon yamefutiliwa mbali baada ya kuchapwa na Venus Williams wa Marekani katika hatua ya nusu fainali.
Venus mwenye miaka 37 alicheza kwa umakini mkubwa zaidi na kushinda kwa seti 6-4 6-2.
Konta anayeshikilia nafasi ya sita kwa ubora duniani, alitegemea kufika fainali hizo na kuwa wa kwanza kufanya hivyo kwa Uingereza tokea mwaka 1977.
Konta anasema alitegemea upinzani mkali kutoka kwa Venus
Matumaini pekee kwa Konta ni kuingia ndani ya tano bora kwa ubora.
Venus atachuana na Garbine Muguruza wa Hispania aliyemchapa Magdalena Rybarikova wa Slovakia kwa seti 6-1 6-1.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive