Monday 24 July 2017

MBOTO: MZEE MAJUTO AJAFA



MSANII wa filamu nchini, Haji Salum maarufu kama Mboto, amekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni zinazodai kuwa nguli wa Vichekesho katika tasnia ya uigizaji, Amri Athuman maarufu kama King Majuto amefariki dunia.
Mboto baada ya kupata taarifa hizi alifunga safari kuelekea mkoani Tanga ambapo ni nyumbani kwa Mzee Majuto na kumkuta hai, na amekanusha uvumi huo kupitia ukurasa wake wa Instagram  kwa kuposti picha inayowaonyesha yeye na Majuto  wakiwa nyumbani kwake, na picha hiyo iliambatana na maneno yafuatayo:
Baada ya kupata taarifa mbaya kuhusu Mzee Majuto nimelazimika kuja kwake Tanga. Ni kweli anaumwa ila anaendelea vizuri na si kama watu walivyozusha kuwa mzee hatunaye. Kwa sasa mzee ni mzima nipo naye Tanga,” ameandika Mboto.
Siku chache zilizopita, Ushindi Media ililiripoti taarifa za kuumwa kwa Mzee Majuto, anayesumbuliwa na tatizo la ngiri, lakini jana kwenye mitandao ya kijamii zikaenea taarifa zisizo za kweli kwamba King Majuto amefariki dunia.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive