Monday 19 June 2017

Trump na familia yake warejea Ikulu





Na Denis Massawe
 
Rais wa Marekani Donald Trump amerejea kwenye Ikulu ya nchi hiyo siku ya Jumapili mchana baada ya kutoka mapumnzikoni alikosheherekea siku ya baba duniani.

Trump alitumia siku ya baba duniani kwenda Camp David tofauti na ilivyozoeleka kwa marais waliopita kwani wengi wao walikuwa wakipumzika maeneo ya Maryland ambako ni mahususi kwa ajili yao.

Katika safari hiyo rais Trump aliambatana na mkewe Melania pamoja na mwanae Barron ambapo Melania alivaa blauzi nyeupe  mchanganyiko na Mizeituni, Maria Jeans na viatu aina ya Manolo Blahnik.


Nae Barron alivaa kawaida tu yaani Jeans, tisheti nyekundu ya Ralph Lauren na sneakers nyekundu vinavyolingana.
Safari hiyo Trump aliifanya kama siri kwani alionekana kutolipenda eneo hilo lililotengwa maalumu kwa ajili ya viongozi wakubwa wa serikali ya nchi hiyo kupumzika.

Eneo hilo ambalo rais huyo iliipeleka familiya yake lilionekana kupedwa sana kwani mkewe Melania alituama ujumbe mfupi kwenye mtandao wa Twitter mwishoni mwa Jumamosi  uliosomeka kuwa 'Barron, @POTUS na ninafurahia Camp David nzuri! #family #sport #weekend.'
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive