Sherehe ya kula nyama ya mbwa
iliogubikwa na utata katika mji wa Yullin nchini China imeanza licha ya
ripoti za awali ilionesha kuwa ilikuwa imepigwa marufuku mwaka huu.
Sherehe hiyo hufanyika kila mwaka katika mkoa wa Guangxi.
Mapema mwaka huu ,wanaharakati walidai kwamba wafanyibiashara waliagizwa na mamlaka kutouza nyama ya mbwa.
Lakini wamiliki wa vibanda vinavyouza nyama hiyo waliambia shirika la BBC hawajasikia lolote kuhusu hatua hiyo kutoka kwa maafisa.
Mnamo tarehe 15 mwezi Mei, maafisa wa mji walithibitisha kwamba hakuna marufuku yoyote.
Siku ya Jumatano, ripoti kutoka Yullin zilisema kuwa
mbwa waliokufa walionekana wakiwa wametundikwa katika ndoano za nyama
katika vibanda ndani ya soko la Dongkou ambalo ndio kubwa mjini humo.
Mwanaharakati
mmoja aliambia shirika la BBC kwamba alikatazwa na maafisa wa polisi kuingia
katika soko la Dashichang ambapo inaaminika mbwa walikuwa wanauzwa.
Katika
sherehe za miaka ya nyuma kumekuwa na mzozo kati ya wauzaji nyama ya
mbwa na wanaharakati waliojaribu kuwaokoa mbwa waliopangiwa kuchinjwa.
0 comments:
Post a Comment