Wednesday 21 June 2017

MFALME WA SAUDIA AMTIMUA MRITHI WAKE

Mfalme Salman wa Saudia

Mfalme Salman wa Saudia amebadilisha mkondo wa urithi na kumfanya mwanawe wa kiume Mohammed bin Salman kuwa mwanamfalme na kuwa wa kwanza kumrithi.

Aliyekuwa mwanamfalme Mohammed bin Nayef amepokonywa taji lake na kufutwa kazi kama waziri wa maswala ya ndani.
Mohammed bin Salman mwenye umri wa miaka 31 ataendelea kuwa waziri wa ulinzi mbali na kuwa naibu waziri mkuu.
Mabadiliko hayo yalitangazwa katika misururu ya amri za kifalme.


 Mwana mpya wa mfalme Mohammed Salman (kushoto) akifuatiwa na  Mohammed Nayef alievuliwa.
 Chombo cha habari cha Saudia kimesema kuwa mfalme ametaka raia wa taifa hilo kumtii mwanamfalme huyo mpya siku ya Jumatano.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive