Tuesday 20 June 2017

SALAMU ZA MANARA KWA WANAYANGA JUU YA MSIBA MZITO ULIYOWAFIKA


 Mabingwa wa soka Tanzania bara kwa mara tatu mfululizo klabu ya Yanga wamepatwa na msiba mzito baada ya moja ya aliyekuwa mshabiki wao nguli kufariki.

Ally Yanga kama anavyofahamika amefariki hii leo mchana jijini Dodoma ambako taarifa zinasema alikuwa kwenye shughuli za kukimbiza mwenge.
Yanga alikuwa maarufu sana katika ushangiliaji kutokana na aina yake ya kipekee ya kujipaka mkaa usoni na kujaza nguo katika tumbo lake kama ana kitambi.
Kutokana na msiba huo aliyekuwa msemaji wa klabu ya Simba bwana Haji Manara ametuma salamu za pole kwa watani wake hao na akisema amehuzunishwa na msiba huo.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram aliandika “nimepigiwa simu kwamba Ally Yanga amefariki huko Mpwapwa mkoani Dodoma,msiba huu ni wetu wote na tunawapa pole watani zetu.”
Ushindi Media inatoa pole kwa Wanayanga wote pamoja na familia ya Ally kutokana na msiba huu mzito “Bwana ametoa na Bwana ametwa jina lake lihimidiwe”.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive