Mahakama ya juu zaidi nchini Afrika Kusini imeamuru kuwa kura ya kutokuwa na imani na Rais Jacob Zuma inaweza kufanywa kwa siri.
Mahakama ya katiba
ilisema kuwa spika wa bunge na haki ya kuamuru hatua kama hiyo. Awali
alisema kuwa hakuwa na mamlaka kama hiyo.
Vyama vya upnzani vinaamini kuwa chini ya kura ya siri, wabunge kutokla chama cha Zuma cha ANC wanaweza kupiga kura ya kumpinga.
Zuma aliponea kura za awaliaza kutokuwa na im,ni naye.
Bwana Zuma amekuwa chini ya shinikizo kufuatia shutuma nyingi
ikiwemo madai ya ufisadi na mabadiliko kwa baraza la mawaziri
yaliyokumbwa na utata.
Akitoa uamuzi huo Jaji mkuu Mgoeng Mgoeng, alisema kuwa spika wa bunge ana mamlaka ya kuamua ni njia gani kura hiyo itafanyika.
Spika
wa bunge Baleka Mbete ni afisa wa juu wa ANC na alikuwa amedai
kuwa sheria za bunge haziruhusu kufanyika kura ya siri,
Sasa tarehe mpya ya kura hiyo ya kutokuwa na imani itatangazwa.
0 comments:
Post a Comment