Marekani imeishinikiza China
kuongeza jitihada zake katika kuizuia Korea Kaskazini kuendelea na
mipango yake ya kinyuklia pamoja na utengezaji wa makombora.
Akizungumza
baada ya kukutana na maafisa wakuu wa China, waziri wa maswala ya
kigeni nchini Marekani Rex Tillerson amesema kuwa Beijing ina jukumu la
kidiplomasia kuongeza shinikizo zaidi kwa Pyongyang iwapo ingetaka
kupunguza wasiwasi katika eneo hilo.
Katika mkutano huo mjini Washington ambao ulihudhuriwa na waziri
wa Ulinzi wa Marekani James Mattis bwana Tillerson alisema kuwa China
inaunga mkono mpango wa Marekani wa kusitisha mpango wa kinyuklia wa
Korea Kaskazini pamoja na majaribio ya makombora ya masafa marefu.
Pia
ameyataka mataifa yote kuongeza juhudi za kumaliza biashara ya kihalifu
ya Korea Kaskazini ambayo anasema inatumika kufadhili mipango yake ya
Kinyuklia.
0 comments:
Post a Comment