Tuesday 24 January 2017

WALICHOSEMA POLISI JUU YA KUKAMATA GARI LA ZITTO KABWE


Kuna taarifa zilienea kwamba Jeshi la polisi Shinyanga linamshikilia kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo na Mbunge wa Kigoma mjini Zitto Kabwe kwa tuhuma za kutoa lugha za uchochezi dhidi ya Rais Magufuli kutokana na ile video fupi inayosambaa.
Ili kuufahamu ukweli,  AyoTV zimemtafuta kaimu kamishna wa Polisi Shinyanga Elias Mwita ambaye amekubali kujibu maswali na kusema Zitto hajashikiliwa na Polisi, kilichofanya waanze kumtafuta Zitto Kabwe ni kuambiwa kwamba anamiliki gari ambalo halina vibali halali.
SWALI: Kuna taaarifa kwamba Polisi walivamia kwenye mkutano wa hadhara aliokuwemo Zitto Kahama, kipi mlichokua mkikitafuta haswa?
JIBU LA POLISI: Hiyo ni kweli na ni baada ya Polisi kupata taarifa za kiintelijensia kwamba Zitto anamiliki gari ambalo halina vibali halali lakini kabla hatujakutana nae Zitto Kabwe akawa ametoweka kwenye eneo hilo na kulitelekeza lile gari, baadae alipatikana Dereva wake tukaomba hizo documents na hazikuwepo’
SOURCE: AYO TV
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive