Friday 20 January 2017

KWA HERI OBAMA NA KIKAPU CHAKO SASANI TRUMP NA MIELEKA YAKE




Leo ndio siku ambapo rasmi raisi Barack Obama anaondoka ikulu,Donald Trump anaenda White House baada ya kuchaguliwa na wananchi wa Marekani.Maraisi wote hawa wana upenzi katika michezo huku Obama akiwa katika kikapu lakini kama hujui nikujuze kuwa Trump ni kati ya watu waliowahi kuwekeza pesa nyingi katika michezo haswa wa mieleka.
Obama anaondoka Marekani akiwa raisi ambae alikuwa kipenzi cha watu wengi duniani.Obama alikuwa mpenda michezo na kama ilivyo ada ya Wamarekani mchezo kwa kikapu ndio mchezo wao mkuu.Akiwa White House Obama alipata nafasi kuzialika timu mbali mbali za kikapu.
Mwaka 2012 Barack Obama alikutana na timu ya kikapu ya Dallas Mavericks,abapo katika mualiko huo mchezaji wa Dallas Dalonte West aliishia getini.West alishindwa kuingia kuonana na Obama kutokana na kuwa na rekodi ya kumiliki silaha kinyume cha sheria.
Lakini mwaka jana pia mwezi wa 11 mabingwa wa ligi ya kikapu ya NBA Cleveland Cavariels wakiongozwa na Lebron James walienda White House kwa mwaliko maalumu kukutana na Barack Obama.Baada ya kuwafunga wapinzani wao Golden State Warriors timu hiyo ilifunga safari hadi kwa Obama hiyo ikiwa siku mbili kabla ya uchaguzi wa Marekani.
Lakini Golden State Warriors pamoja na kufungwa na Cavs ila wao walishatangulia ikulu kabla yao kwani April mwaka jana wakiwa na Steph Curry walienda hadi ikulu kukutana na raisi Obama.
Obama hakuwa anajua kuhusu kikapu tu hata soka pia yumo,ambapo mwanae Sasha ni shabiki mkubwa wa Lioneil Messi.March mwaka 2016 mchezaji wa Argentina Lioneil Messi alisema anatamani kukutana na raisi Barack Obama.Messi aliongea haya baada ya mtoto wa Obama aitwaye Sasha kumuambia baba yake kwamba anatamani kumuona Messi.Katika ziara yake nchini Argentina Obama aliwaeleza watu kuhusu tamanio hilo la mtoto wake.
Obama hakuanza kumjua Messi hapi kwani mwaka 2011 wakati akipewa jezi namba 10 kutoka timu ya Colorado Rapids Obama aliwatania Colarado na kusema “nashukuru munajua kuwa namba 10 ndio kiongozi kwahiyo mimi na messi ni viongozi”
Lakini katika utawala wa Obama Manchester United pia walitembelea White House.Hiyo ilikuwa mwaka 2011 lakini kutokana na majukumu Obama alishindwa kukutana na timu hiyo.
Sasa anakuja Donald Trump mfanyabiashara mkubwa ambae ameshawahi kuinvest pesa kubwa sana katika mieleka.Kuanzia leo Trump anaingia madarakani baada ya kuchaguliwa na wananchi wa taifa hilo kuliongoza.Pengine hujui au umesahau kuhusu Trump na WWE(World Wrestling Entertiment)basi  leo tunakujuza na kukumbusha.
Mwaka 2007 katika plaza ya Trump iitwayo Donald Trump Plaza iliyokohuko New Jersey iliandaa mpambano wa Wrestlmenia IV na Wrestlmenia V na plaza hiyo kuingia katika historia ya shoo hiyo kwa kuiandaa mara mbili katika miaka miwili mfululizo.
Katika mwaka huo mwezi January Trump alimtibua mwenyekiti wa WWE MR.McMahons katika usiku ulioiywa “Night Of Apreciation”.Trump alirusha dola elfu kumi katika uwanja huo kwa mashabiki.Mcmahon hakukubali aliitisha mpambano ulioitwa “Battle Of Billionaires” katika pambano hilo kila bilionea alichagua mpiganaji wake na mpiganaji wako akishindwa unanyolewa nywele.Pambano hili liliisha kwa mpiganaji wa Trump aitwae Bob Rashley kudshinda dhidi ya Umaga wa Mcmahon na hivyo Trump kumnyoa Mcmahon nywele mbele za watu.
Trump ana historia kubwa na mieleka,mwaka 2009 yeye ndiye alikua akiandaa usiku wa mieleka ujulikanao kama Monday night raw.Trump anaingia madarakani sasa sijui kama atauacha moja kwa moja uhusiano wake na mieleka.Lakini pia haitakuwa ajabu kuwaona kina John Cena na Undertaker kuhudhuria White house kwa wingi.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive