Thursday, 3 November 2016

DC KIGAMBONI AWAWEKA NDANI WAZAZI WA WANAFUNZI WATORO




Mkuu wa wilaya ya Kigamboni Hashim Mgandilwa ameanza ziara ya kutembelea Kata za Wilaya ya Kigamboni, ambapo ameanzia Kata ya Kimbiji na kuzindua vyumba vitatu vya madarasa katika shule ya msingi Bohari.dc-hashimu-kigamboni-students-1

Mapema akizindua vyumba vya madarasa DC Mgandilwa aliingia madarasani na kukuta mahudhurio ya wanafunzi hayaridhishi huku kukiwa hamna taarifa yoyote kwa Mwalimu Mkuu juu ya ruhusa au wanafunzi wagonjwa.dc-hashimu-kigamboni-students-5

Kufuatia utoro huo wa wanafunzi DC Mgandilwa amewaweka ndani wazazi (2) wa wanafunzi hao na kuagiza wazazi wengine wa wanafunzi watoro ambao hawakuwepo mkutanoni kutafutwa na  kukamatwa kwani utoro huo unasababishwa na wazazi.dc-hashimu-kigamboni-students-6

Ziara aliyoianza leo DC Mgandilwa inalenga kushirikiana na wananchi katika shughuli za kimaendeleo, kusikiliza na kutatua kero zao moja kwa moja katika maeneo wanayoishi.dc-hashimu-kigamboni-students-4

Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive