Thursday, 3 November 2016

TAARIFA KUSUHU KUPUNGUA KWA VIFO WAZAZI NA WATOTO


Tanzania imepiga hatua kubwa katika kuboresha huduma za uzazi wa mpango nchini tofauti na kipindi cha nyuma ili kuweza kuondoa idadi ya ongezeko kubwa la watu na kupunguza vifo kwa wajawazito na watoto kama Sera ya Afya ya mwaka 2007 inavyosema.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati akifungua mkutano wa bodi kwa nchi zilizoamua kuongeza idadi ya watu wanaofahamu uzazi wa mpango kundi linalojulikana kama “FP 2020 Reference Group”.ummy mwalimu

“Tanzania imepiga hatua kubwa katika kuboresha huduma za uzazi wa mpango nchini tofauti na kipindi cha nyuma ili kuweza kuondoa idadi ya ongezeko kubwa la watu na kupunguza vifo kwa wajawazito na watoto kama sera ya Afya ya mwaka 2007 inavyosema” amesema Waziri Ummy.

Aidha Waziri Ummy amesema mkutano huu unafanyika kwa mara ya kwanza barani Afrika na hususani katika ardhi ya Tanzania hii ni kutokana na mafanikio makubwa yaliyofikiwa katika eneo hili la uzazi wa mpango . Mkutano huo wa siku tano ulioanza Oktoba 31 hadi  Novemba 4 mwaka huu unahudhuriwa na wajumbe na wadau kutoka nchi mbalimbali duniani ikiwa na lengo la kujadili fursa mbalimbali na changamoto zilizopo katika eneo la afya ya uzazi wa mpango duniani.

Waziri Ummy amesema mafanikio hayo ni pamoja na ongezeko la bajeti katika eneo la uzazi wa mpango na kupunguza hali ya utegemezi kwa kiasi kikubwa kutoka kwa wahisani, kuimarisha mìfumo ya usambazaji wa dawa na vifaa tiba za uzazi wa mpango hapa nchini.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalosimamia masuala ya uzazi wa mpango Dk. Babatunde  amepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali ya  Tanzania katika kuhakikisha huduma hii inaimarika.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive