Thursday, 3 November 2016

AGIZO LA JPM LAWATOA JASHO WAHUDUMU WA VYOO



AGIZO la Rais John Magufuli la kuwataka wananchi kudai au kutoa risiti pindi wanapouza au kununua bidhaa, limewatoa jasho wafanyabiashara wanaotoa huduma za choo katika jiji la Mwanza.

Katika kutekeleza agizo hilo, wafanyabiashara hao wamesema wananchi wanaopata huduma katika baadhi ya vyoo vya kulipia, wamekuwa wakitaka wapewe risiti za kielektroniki (EFD) badala ya zile za karatasi.

Hatua hiyo imetokana na baadhi ya wazabuni wanaoendesha huduma za vyoo kutumia risiti za Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa kuwa vyoo hivyo viko chini ya halmashauri hiyo.

Msimamizi wa choo kilichoko maeneo ya Makoroboi, jijini hapa, Masoud Masib, alisema wao wanatumia risiti kutoka Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa sababu vyoo hivyo viko chini ya halmashauri.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive