Sunday 8 October 2017

HII NDIYO SIKU YA OKWI KUREJEA SIMBA

Mchezaji wa Simba, Emmanuel Okwi.
Mshambuliaji nyota wa Simba na mchezaji bora wa mwezi, Emmanuel Okwi anatarajia kurejea nchini ili kuungana na klabu yake ya Simba siku ya kesho akitokea nchini Uganda.
 
Okwi aliondoka nchini kwenda Uganda ambako aliungana na kikosi cha timu ya taifa ya Uganda kwa ajili ya mechi ya kuwania kufuzu kucheza Kombe la Dunia.

Katika mechi hiyo, Uganda ilifanikiwa kupata sare ya bila kufungana, mechi ambayo ilikuwa ngumu.

Maofisa wa Simba wamesema, Okwi atangana na wenzake kesho kwa ajili ya maandalizi ya mechi zijazo.


Simba inatarajia kuivaa Mtibwa Sugar katika mechi ijayo ya Ligi Kuu Bara, mechi itakayopigwa Jumapili ijayo.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive