Sunday 10 September 2017

WENGER ASEMA HAYA KUHUSU MBAPPE

Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger amesema kipaji cha Kylian Mbappe ni kikubwa na anamfananisha mchezaji huyo na nguli wa zamani wa Brazil, Pele. 

Wenger amesema kuwa anaamini PSG imefanya maamuzi sahihi kumsajili mchezaji huyo na anaweza kuwa  mchezaji bora wa dunia.


“Nafikiri ni mchezaji mwenye kipaji cha juu, ana sifa nyingi za kuwa bora, ni Pele mpya.
 Mbappe ambaye ametua PSG akitokea Monaco alifunga bao moja katika mechi yake ya kwanza akiitumikia timu yake mpya juzi ilipoifunga Metz mabao 5-1 katika Ligue 1.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive