Friday 8 September 2017

MKATABA WA MANULA WAMTIMUA MGHANA SIMBA

IMEBAINIKA kuwa mkataba wa kipa, Aishi Manula ndani ya klabu ya Simba ndiyo uliochangia timu hiyo kuachana na kipa Mghana, Daniel Agyei.
Beki wa kati wa Azam FC, Yakubu Mohammed ameiambia Mwanaspoti kuwa walimsihi Manula asiende Simba kwani angeshindwa kutamba mbele ya Agyei lakini aling'ang'ania kwa kuwa alifahamu mpinzani wake huyo ataondolewa.
"Agyei ni kipa makini, hata rekodi zake zilikuwa vizuri. Tulipoona Manula anakwenda Simba tulimshauri asiende kwani angepata ushindani mkubwa kutoka kwake, nadhani alifahamu kwamba ataondolewa," alisema Mohammed.
"Kama Agyei angebaki ushindani ungekuwa mkubwa zaidi, Simba pia wangekuwa vizuri zaidi. Kwa sasa Manula ana uhakika wa kuanza kila mechi," alifafanua.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive