Sunday 17 September 2017

KUWAIT YAFUTA UBALOZI WA KOREA KASKAZINI

Emir wa Kuwaiti, Sheikh Sabah al-Ahmad Al-Sabah, akizungumza na waandishi wa habari alipokutana na raisi wa Marekani, Donald Trump,katika ikulu ya nchi hiyo iliyopo Washington, DC, Septemba  7, 2017. (AFP photo)
Ripoti kutoka nchini Kuwait zinasema kuwa imemfukuza balozi wa Korea Kaskazini.
Hakuna taarifa rasmi iliyotolewa lakini kuwait imewaambia waandishi wa habari kuwa balozi wa Korea Kaskazini, amepewa mwezi mmoja kuondoka huku wanadiplomaisa wa Korea Kaskazini wakipunguzwa.
Kuwait ndiyo nchi pekee katika ghuba iliyo na ubalozi wa Korea Kaskazini.
Maelfu ya raia wa Korea Kaskazini wanafanya kazi nchini kuwait na nchi zingine za ghuba kama vibarua.
Hatua hiyo inachukuliwa wiki mbili baada ya kiongozi wa kuwait kuzuru Washington.
Marekani imetaka hatua za kimataifa kuchukuliwa dhidi ya Korea Kaskazini kufuatia mipango yake ya nyuklia.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive