Saturday 30 September 2017

ALICHOSEMA MANARA LEO CHAZUA GUMZO MTANDAONI

 Afisa habari wa klabu ya Simba, Haji Manara amezua gumzo mtandaoni leo baada ya kufunguka jambo lililoonekana kuwa mwiba mkali kwa mashabiki wa Yanga, Azam na Simba.

Msemaji huyo wa wekundu wa msimbazi alidai kuwa kitendo cha mchezaji, Cristiano Ronaldo kununua gari aina ya bugatti lenye thamani ya bilioni nne za kitanzania ni ukatili uliopitiliza bora pesa hizo zingetumika kulipa wachezaji wa Yanga, Simba na Azam.
Manara alieleza hayo kupitia ukurasa wake maalum wa instagram baada ya kupita siku moja tokea nyota huyo wa kimataifa anayechezea klabu ya Real Madrid kuweka hadharani gari hilo katika mtandao wake na kufanya mamia ya watu kumpongeza kwa hatua hiyo aliyofikia huku wengine wakibakia kutoamini kwa kilichotokea.

"Bugatti ya 2017 imenunuliwa na Ronaldo kwa thamani ya Dola milion 1.8, karibia na Bilioni nne za madafu. Unalipa 'salary' ya mwaka mzima kwa wachezaji wa Yanga, Simba na Azam. Huu ni ukatili uliopitiliza", ameandika Manara.
Hivyo Manara akajikuta akiwaacha mashabiki wa timu za hapa nchini katika mzozo usio na kikomo.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive