Tuesday 29 August 2017

TFF WATETA JUU YA CHIRWA, KASEKE

Hatma ya wachezaji kiungo wa Singida United Deus Kaseke na mshambuliaji wa Yanga, Obrey Chirwa itajulikana alhamis ijayo baada ya kikao cha kamati ya saa 72.
Kaseke na Chirwa walismamishwa kucheza baada ya kutuhumiwa kufanya fujo katika mechi ya mwisho ya Ligi Kuu msimu uliopita katia ya Yanga dhidi ya Mbao FC.
Ofisa Habari wa TFF alisema kikao hicho kitatoa uamuzi juu ya shauri hilo.
"Kikao kimechelewa kwa sababu ya uchaguzi na kubadilishwa kwa kamati za TFF, lakini mtakumbuka wachezaji hawa walisimamishwa kwenye mechi ya mwisho msimu uliopita,"alisema Lucas.
Kutokana na adhabu hiyo Kaseke alikuwa jukwaani wakati Singida United ikipokea kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Mwadui, kama ilivyokuwa kwa Mzambia Chirwa aliyeshindwa kuichezea Yanga katika mechi ya Ngao ya Jamii dhidi ya Simba pamoja na mechi ligi dhidi ya Lipuli wakitoka sare 1-1.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive