Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA na Mbunge wa
Singida Mashariki, Tundu Lissu amechukuliwa na Polisi wakati akitokea
Mahakamani akitakiwa Kituo Kikuu cha Polisi baada ya kumaliza shughuli
za Mahakamani.
Tundu Lissu alikuwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwenye
kesi ya uchochezi inayomkabili lakini pia alikuwa Wakili kwenye kesi ya
Yericko Nyerere.
Msemaji wa CHADEMA Tumaini Makene amesema kuwa wakati gari la Lissu
likiwa getini tayari kutoka eneo la Mahakama baada kumaliza shughuli za
Mahakama lilisimamishwa na Polisi ambao baadhi walimfuata na kumwambia
yuko chini ya ulinzi na kutakiwa kwenda Central Police.
0 comments:
Post a Comment