Monday 7 August 2017

OKWI NA NIYONZIMA MSIMBAZI HAPATOSHI


Image result for OKWI VS NIYONZIMA

 Simba imewatambulisha  wachezaji wake wapya Emmanuel Okwi, Haruna Niyonzima pamoja na Mghana  Nicholaus Gyan kabla ya kutembelea Taasisi  ya  Moyo ya Jakaya Kikwete.
Wakizungumza katika mkutano huo nahodha wa  Simba, Method Mwanjali, Okwi pamoja na  Niyonzima waliwashukuru wanachama wa klabu  kwa kuwapokea vizuri na kuahidi kuleta mafanikio katika timu hiyo.
Afisa habari wa Simba, Haji Manara  aliwatambulisha wachezaji Okwi, Niyonzima na Gyan mbele ya wanahabari.
Manara wachezaji hao watatambulishwa rasmini  kwa mashabiki kesho katika tamasha Simba Day ambalo mgeni rasmi atakuwa Waziri wa Mazingira, January Makamba.
"Kesho tutawatambulisha rasmi wachezaji wetu wote wapya na tunategemea watacheza mechi hiyo." Siku ya kesho, Simba itacheza mechi ya kirafiki na Rayon Sports ya Rwanda wakati mchezo wa mapema utawakutanisha Simba B dhidi ya Vijana Rangers.
Kabla ya mchezo huo kuanza mechezo bora wa Ligi Kuu Bara, beki Mohamed Hussein atakabidhiwa tuzo yake.
Tuzo hiyo inatokana na kura za mashabiki wa Simba waliopiga kumchagua mchezaji bora wa msimu uliopita.
Mashabiki wa Simba wataanza kuingia uwanja wa Taifa kuanzia saa 4 asubuhi, watapata burudani za kutosha kutoka kwa wasanii  mbalimbali.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive