BAADHI
ya mahujaji waliokuwa wamejiandaa kwa ajili kwenda Mecca nchini Saudi
Arabia, wamekwama katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere
Dar kufuatia visa, passport na tiketi zao kutokuwa tayari kwa ajili ya
safari hiyo.
Wakizungumza LIVE na moja ya vyombo vya habari hapa nchini,
mahujaji hao wamesema walitakiwa kuondoka hapa nchini kuelekea Mecca na
ndege ya saa 8 mchana lakini cha kushangaza imeshindikana kwa kuwa
taasisi walioilipa fedha ili kuwakamilishia taratibu zote za safari hiyo
viongozi wake wameingia mitini na kuwaachia mabegi matupu.
Mahujaji hao wanaeleza kusikitishwa
kwao na kile walichokiita kuwa ni utapeli huku wakifanya kila jitihada
za kuwasiliana na viongozi wa taasisi hiyo lakini simu zao hazipokelewi
na wengine zinapokelewa na wafanyakazi wao wa ndai huku wakiwaeleza kuwa
wahusika wa simu hizo hawapo jambo ambalo wameshindwa cha kufanya,
hivyo wameamua kwenda kituo cha polisi kutoa taarifa.
0 comments:
Post a Comment